Tuesday, September 07, 2010
   
Text Size

Site Search

Manji! Ee bwana ee!

*Anunua tiketi za Sh milioni 90 kwa ajili ya wanachama wa Yanga kuiona Stars ikikipiga na Brazil wiki ijayo

Na Mwandishi Wetu

HATIMAYE ahadi ya mdhamini wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji imetimia na sasa wanachama 3,000 wa klabu hiyo wana uhakika wa kuiona mechi kati ya Taifa Stars na Brazil Jumatatu ijayo.

Mfanyabiashara huyo kijana jana alinunua tiketi hizo zinazouzwa kwa Sh 30,000 kila moja hivyo kuwa na jumla ya thamani ya Sh milioni 90, zitakazogawiwa kwa wanachama watakaohudhuria Mkutano Mkuu wa utakaojadili rasimu ya Katiba ya klabu hiyo, Jumatatu ijayo kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay.

Barua aliyomwandikia Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), yenye kumbukumbu namba Yanga.TR/ 042.010 ya jana, inaonyesha kuwa Manji anaiomba TFF kumpatia tiketi 3,000 kwa ajili ya wanachama wa Yanga ili wakaishangilie timu ya taifa itakapocheza na Brazil.

Ni wazi kuwa TFF ililikubali ombi hilo kwani Manji alipa fedha kwa ajili ya tiketi hizo kwenye tawi la CRDB, Pugu Road jijini hapa.

Manji alilipa kwa hundi ambazo nakala zake tunazo, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mdhamini mmoja kununua idadi kubwa namna hiyo ya tiketi.

Hii si mara ya kwanza kwa ‘kibopa’ huyo kufanya kufuru kwani alipokuwa mfadhili wa Yanga, aliwahi kuwaingiza bure mashabiki wa timu hiyo kwenda kuishangilia timu yao ilipokuwa ikicheza mechi moja ya kimataifa kwenye Uwanja wa Kirumba, Mwanza.

Kitendo hicho cha Manji ni katika harakati zake za kuhakikisha mkutano huo muhimu utakaotengeneza njia ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa klabu hiyo, unafanikiwa huku ukiwa wa amani.

More Latest News

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4

cartoons



Who's Online

We have 14 guests online

Login Form