Kipa mpya Yanga kutua leo
NA TIMZOO KALUGIRA
MRITHI wa kipa namba moja wa Yanga, Obren Curkovic anatarajia kutua leo akiwa na Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mserbia Costadin Papic.
Kipa huyo ambaye pia kutoka Serbia anaitwa Knezevic Ivan anakuja baada ya Obren kumaliza mkataba wake na klabu hiyo na kukataa kuongeza.
Obren aliondoka hapa nchini mara baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu Tanzania Bara msimu wa 2009/2010.
Habari za kuaminika kutoka ndani ya klabu hiyo zilisema kuwa wakati Papic akiwa likizo alimtafuta kipa huyo ili kuja kuwa na mlinda mlango wa uhakika.
“Kipa huyo anakuja kesho (leo) na kocha hivyo atafika na kusaini mkataba ingawa bado sijajua atasaini mkataba wa miaka mingapi,” kilisema chanzo hicho.
Aidha alisema kuwa baada ya kutua kocha, timu inatarajia kuanza mazoezi keshokutwa.
Wakati huo huo Katibu Mkuu wa Yanga Lawrance Mwalusako, jana alizindua tawi la Yanga Lango la Jiji ambalo litatumia jina la mpira mbinu.
Hata hivyo wakati wa uzinduzi wa tawi hlo hakukuwa na shamra shamra sana na badaka yake wanatarajia kufanya sherehe hapo baadaye.
More Latest News
-
Daladala latumbukia mtoni Dar ABIRIA 21 waliokuwa wakisafiri kutoka Buguruni kwenda Mbagala jijini...
-
Umeyasikia ya Tatu Ntimizi? BAADHI ya wananchi wa Jimbo la Igalula ambao ni wanachama wa Chama...
-
Hispania yaweka historia HISPANIA imekuwa taifa la nane kushinda Kombe la Dunia baada...
- 1
- 2
- 3
- 4
Advertisement

cartoons


