Friday, September 10, 2010
   
Text Size

Site Search

Humud akwama kwenda Urusi

NA TIMZOO KALUGIRA

MABINGWA wa soka wa Ligi Kuu ya Bara, Simba ya Dar es Salaam wanadaiwa kuzuia kiungo wao, Abdulhalim Humud kwenda nchini Urusi kufanya majaribio ya soka la kulipwa.
Habari ambazo Bingwa imezipata kutoka kwa mtu wa karibu na mchezaji huyo zinadai kwamba kuna timu nchini Urusi ilikuwa ikimtaka mchezaji huyo lakini viongozi wake walimkatalia.
“Jambo hili lilimkera mno Humud ameonekana kukosa raha baada ya kukataliwa kwenda kusakata kandanda huko Urusi, aliwambia viongozi wake kuwa kama vipi waongee na timu hiyo wapande dau kwa kulipa mkataba aliokuwa nao lakini walimkatalia,” alisema mtoa habari hiyo.
Mtoa habari hiyo aliliarifu Bingwa kuwa kutokana na kuwa na mkataba na klabu hiyo ilimbidi akubaliane na hali halisi kwani hakuna kiongozi hata mmoja aliyekuwa tayari kushughulikia suala lake.
Bingwa lilimtafuta Humud ili kuzungumzia suala hilo lakini mchezaji huyo alisema kuwa kwa sasa hayuko tayari kuzungumzia mambo hayo na anachokiangalia ni msimu mpya wa ligi inayotarajia kuanza Agosti mwaka huu.
Hata alipobanwa na Bingwa, mchezaji huyo badala yake alionekana kuihimiza kamati ya usajili ya klabu hiyo, kusajili wachezaji wa maana wanaoweza kuisaidia timu iweze kutetea ubingwa msimu ujao.
“Kamati iangalie ni wapi palikuwa na mapungufu timu ilipokuwa uwanjani katika msimu uliopita, ili kuweza kusajili wachezaji wanaoweza kuziba pengo hilo na kuleta maendeleo katika klabu yetu,” alisema Humud.
Bingwa lilizungumza na Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage ambaye hata hivyo alisema kwamba hangependa kuzungumzia vitu visivyo rasmi.
“Hayo mambo si rasmi kwa hiyo sina habari yoyote kuhusu hilo na siwezi kuzungumza chochote,’’ alisema.

More Latest News

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4

cartoons



Who's Online

We have 8 guests online

Login Form