Tuesday, September 07, 2010
   
Text Size

Site Search

dimba

Aliyemvamia Kaka bado asota rumande

Na Tumain Kyomo, DACICO

JESHI la Polisi linaendelea kumshikilia shabiki wa soka ambaye juzi alivamia uwanja na kwenda kumkumbatia Ricardo Kaka wa Brazil ilipokuwa ikiumana na Taifa Stars.
Tukio hilo lililoshangaza wengi lilitokea Uwanja wa Taifa katika mechi hiyo ya kimataifa ya kirafiki, ambapo Stars ilichapwa mabao 5-1.

Kamanda wa Polisi wa Temeke, David Misime, alisema jana kuwa jeshi lake linamshikilia shabiki huyo, Ally Komba (21) ili kumhoji zaidi katika uchunguzi wa suala hilo.
Alisema mahojiano ya awali yanaonyesha Ally ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Green Acres ya jijini Dar es Salaam.


Wakati mechi hiyo iliyovuta hisia za mashabiki wengi nchini ikiendelea, shabiki huyo alichomoka ghafla ya kuingia uwanjani na kwenda kumkumbatia mshambuliaji huyo nyota.


Kwa mujibu wa kanuni za soka, shabiki yeyote haruhusiwi kuingia na kuwakaribia wachezaji katika sehemu ya kuchezea wakati mchezo ukiendelea.
Hata hivyo haikueleweka shabiki huyo alivukaje hadi kuingia uwanjani, kwani askari wa ulinzi walikuwapo.


 

Dunga amsikitikia Maximo

Na Dominic Isiji

KOCHA mkuu wa timu ya soka ya Brazil, Carlos Dunga, ameeleza kusikitishwa kwake na kuondoka kwa kocha mkuu wa timu ya Tanzania, Taifa Stars, Marcio Maximo ambaye mkataba wake unakamilika mwezi ujao.

Tayari Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limemtangaza Jan Poulsen raia wa Denmark kama mrithi wa Maximo na ataingia mkataba wa miaka miwili Agosti Mosi mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam juzi baada ya mechi ya kihistoria kati ya Taifa Stars na mabingwa wa dunia mara tano, Dunga alisema Maximo amefanya kazi kubwa kuibadilisha Taifa Stars.

“Ninampongeza Maximo kwa kazi nzuri aliyofanya kwa timu hii (Taifa Stars) ila cha kusikitisha ni kwamba anamaliza muda wake,” alisema nahodha huyo wa zamani wa Brazil.

Dunga alikiri kufurahishwa na mchezo wa juzi ambao Brazil ilishinda 5-1 akisema kuwa alihitaji kucheza na timu yenye kasi.

Alisema kuwa Maximo ameweza kutengeneza timu nzuri yenye kucheza na mipango na kwa kasi jambo ambalo liliwapa taabu mabeki wake na wakati mwingine kufanya washindwe kupanda wakihofia kuzidiwa kasi kwa mashambulizi ya kushitukiza.

Katika mchezo wa juzi, Brazil ilitumia kikosi chake cha kwanza ambacho kilimkosa mchezaji mmoja tu, kipa Julio Cesar anayeuguza jeraha ya mgongo na alishindwa kusafiri na timu hiyo kuja Dar es Salaam.

Dunga alisema kuwa nia ya Brazil kucheza na Zimbabwe na Tanzania kama maandalizi yao kuelekea Kombe la Dunia linaloanza kesho kutwa nchini Afrika Kusini, ilikuwa ni kujipima nguvu na kasi ya timu pinzani hususan za Afrika.

“Nchi za Afrika zinasifika kuwa na wachezaji wenye nguvu na kasi na nimeridhika na michezo yetu miwili ya kimataifa ya kirafiki kwa sababu Zimbabwe walicheza mpira wa nguvu na Tanzania mpira wa kasi vitu ambavyo wachezaji wangu waliweza kuvimudu,” alisema.

Hadi mechi ya juzi, Brazil mara ya mwisho kwa nyavu zao kutikiswa ilikuwa Oktoba mwaka jana ambapo walishinda 2-1 katika mchezo wao wa kufuzu kuelekea Kombe la Dunia.




Maximo

KOCHA mkuu wa timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, anayemaliza muda wake Marcio Maximo amesema kuwa mrithi wake atapata kazi rahisi.

Nafasi ya Maximo itachukuliwa na Jan Poulsen raia wa Denmark ambaye anatarajiwa kuingia mkataba wa miaka miwili Agosti 1 mwaka huu.

Akizungumza baada ya mechi ya juzi kati ya Taifa Stars na Brazil uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na Rais Jakaya Kikwete, Maximo alisema mrithi wake hatakuwa na shida ya kuanza kuunda kikosi.

Alisema kuwa anaondoka huku akimwachia Poulsen kikosi imara cha Taifa Stars na timu nzuri za vijana.

“Sidhani kama (mrithi wangu) atapata shida na ninategemea kuwa atayaendeleza mazuri niliyoanzisha ila kama atataka kuanza upya, hiyo itakuwa jukumu lake,” alisema Maximo huku akimtakia kila la heri Poulsen .

Akizungumzia kuhusu mechi ya juzi, Maximo alisema amefurahishwa na wachezaji wake licha ya kwamba walilazimika kucheza michezo miwili muhimu ndani ya saa 24.

Stars walifunga na Rwanda 1-0 Jumapili jijini Kigali na kuyaaga michuano ya Kombe la Afrika kwa wachezaji wa ndani (CHAN) kwa jumla ya mabao 2-1 na siku iliyofwata wakafungwa 5-1 na mabingwa wa dunia mara tano Brazil katika mechi ya kihistoria.

Maximo alisema ijapokuwa anaondoka, matarajio yake ni kwamba Taifa Stars itacheza mechi nyingi za kirafiki kama ile ya Brazil ili kuwakomoza wachezaji.

Alisema kuwa mechi dhidi ya Brazil ilikuwa darasa tosha ya ni nini kinachotakiwa kwa wachezaji ili nao pia waweze kucheza soka la kulipwa.

 

Manji! Ee bwana ee!

*Anunua tiketi za Sh milioni 90 kwa ajili ya wanachama wa Yanga kuiona Stars ikikipiga na Brazil wiki ijayo

Na Mwandishi Wetu

HATIMAYE ahadi ya mdhamini wa klabu ya Yanga, Yusuph Manji imetimia na sasa wanachama 3,000 wa klabu hiyo wana uhakika wa kuiona mechi kati ya Taifa Stars na Brazil Jumatatu ijayo.

Mfanyabiashara huyo kijana jana alinunua tiketi hizo zinazouzwa kwa Sh 30,000 kila moja hivyo kuwa na jumla ya thamani ya Sh milioni 90, zitakazogawiwa kwa wanachama watakaohudhuria Mkutano Mkuu wa utakaojadili rasimu ya Katiba ya klabu hiyo, Jumatatu ijayo kwenye Ukumbi wa Bwalo la Maofisa wa Polisi, Oysterbay.

Barua aliyomwandikia Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), yenye kumbukumbu namba Yanga.TR/ 042.010 ya jana, inaonyesha kuwa Manji anaiomba TFF kumpatia tiketi 3,000 kwa ajili ya wanachama wa Yanga ili wakaishangilie timu ya taifa itakapocheza na Brazil.

Ni wazi kuwa TFF ililikubali ombi hilo kwani Manji alipa fedha kwa ajili ya tiketi hizo kwenye tawi la CRDB, Pugu Road jijini hapa.

Manji alilipa kwa hundi ambazo nakala zake tunazo, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mdhamini mmoja kununua idadi kubwa namna hiyo ya tiketi.

Hii si mara ya kwanza kwa ‘kibopa’ huyo kufanya kufuru kwani alipokuwa mfadhili wa Yanga, aliwahi kuwaingiza bure mashabiki wa timu hiyo kwenda kuishangilia timu yao ilipokuwa ikicheza mechi moja ya kimataifa kwenye Uwanja wa Kirumba, Mwanza.

Kitendo hicho cha Manji ni katika harakati zake za kuhakikisha mkutano huo muhimu utakaotengeneza njia ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu wa klabu hiyo, unafanikiwa huku ukiwa wa amani.

   

Papic, Yanga hakijaeleweka

na mwandishi wetu

KOCHA mkuu wa Yanga, Kostadin Papic hadi jana bado alikuwa hajajua hatima yake iwapo ataendelea kuinoa timu hiyo kwa msimu ujao au la.

Akizungumza na DIMBA jana, Papic alisema kwamba alitarajia kukutana na viongozi na upande wa mfadhili wa klabu hiyo Yusuph Manji ili kuzungumza suala zima la mkataba wake.
“Leo kila mtu anaonekana kuwa busy (ana kazi nyingi) lakini baadaye jioni tutakuwa na kikao ili nijue nitakavyoendelea kuwa na Yanga kwa msimu ujao,’’ alisema kocha huyo kutoka Serbia.

Alipoulizwa nini matumaini yake kuhusu mazungumzo hayo, Papic alisema kwamba anaamini mambo yanaweza kwenda vizuri katika kikao hicho ingawa alitahadharisha: “Siwezi kusema moja kwa moja kama kila kitu kitakwenda sawa.

“Unajua ni lazima uwe umekamilisha kila kitu ndio ujue kama mambo yamekwenda sawa au la lakini kwa sasa pamoja na matumaini yangu lakini hatujui hali itakuwaje.”

Papic alitangaza kuondoka katika klabu hiyo hivi karibuni kwa kile kilichodaiwa kutoridhishwa kwake na mwenendo mzima wa klabu hiyo ambalo alimlaumu mfadhili wao Manji pamoja na uongozi.

Miongoni mwa mambo aliyokuwa akiyalalamikia kocha huyo aliyewahi kufanya kazi nchini Afrika Kusini na Ghana ni kucheleweshewa haki zake ikiwamo mshahara pamoja na makubaliano kadhaa kutotimizwa katika mkataba wake.

Vyombo vya habari jana vilitawaliwa na habari za kocha huyo kusaini mkataba wa mwaka mmoja lakini mwenyewe amesisitiza kwamba hilo litafanyika baada ya mazungumzo kwenda vizuri
Naye Mwenyekiti wa Yanga, Imani Madega alisema uongozi wake ulikaa jana kuzungumzia masuala kadhaa yanayohusiana na kocha huyo ili kuyamaliza matatizo yote ambayo yalikuwa yanaonekana kutokuwa na muafaka kati ya Manji na Papic.

Alisema uongozi ulikuwa na kikao kizito jana (juzi) cha kusawazisha masuala hayo ya kuondoka kwa kocha huyo ambaye alitua nchini Oktoba mwaka jana na kuchukua nafasi ya mserbia mwenzake, Dusan Kondic.

“Hatutaki kurudi tulikotoka, ninavyozungumza na wewe uongozi umekaa kujadili masuala mbalimbali ambayo yataleta muafaka kati ya Manji na kocha wetu, kwa maana hiyo yaliyopita ambayo mwalimu alikuwa akidai tumeyaacha, tunachoangalia sasa  kubaki kwa kocha wetu,”alisema.
 
Madega aliongeza kwamba anaamini suala la kubaki kwa kocha huyo halitakuwa na ugumu kwa kuwa yeye ni muelewa na ataendelea kuinoa Yanga

 

Maximo: Ngassa anaendelea vizuri

altna timzoo kalugira


MSHAMBULIAJI wa timu ya Taifa, Taifa Stars, Mrisho Ngassa, huenda akacheza mechi dhidi ya Rwanda, baada ya kuonekana hali yake imeanza kuimaRika.

Taifa Stars na Rwanda wanatarajiwa kucheza Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, katika mchezo wa kuwania nafasi ya kufuzu michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (CHAN), inayoshirikisha wachezaji wanaocheza soka la ndani.

Akizungumza na DIMBA juzi, wakati wa mazoezi ya timu hiyo kwenye Uwanja wa Karume jijini, Kocha Mkuu wa Stars, Mbrazil Marcio Maximo, alisema kuwa hali yake kwa sasa inaendelea vizuri na huenda akamtumia siku hiyo.

“Alikuwa anasumbuliwa na malaria, lakini kwa sasa hali yake si mbaya sana, ameanza kufanya mazoezi mepesi na wenzake, japo kuna baadhi ya mazoezi anashindwa kuyamudu kutokana na afya yake kutokuwa nzuri,” alisema Maximo.

Maximo alisema kuwa kama hali itaendelea kuwa nafuu, kuna umuhimu wa kumtumia katika mechi hiyo ili kuongeza nguvu nyingine na kuweza kuibuka na ushindi ili kusonga mbele kwenye michuano hiyo.

Ngassa, ambaye pia ni mshambuliaji wa timu ya Yanga, alikuwa anasumbuliwa na homa ya matumbo (typhoid) pamoja na malaria.

   

Page 1 of 4

More Latest News

  • 1
  • 2
  • 3
  • 4

cartoons



Who's Online

We have 13 guests online

Login Form